IQNA

Siku Kuu

Ni nchi gani zilizotangaza Eid al-Fitr Ijumaa

17:55 - April 21, 2023
Habari ID: 3476896
TEHRAN (IQNA)-Waislamu kote ulimwenguni leo wameanza kusherehekea moja ya karamu zao muhimu zaidi, Idul Fitr.

Nchi kadha zilitangaza kumalizika kwa Ramadhani na kuanza kwa mwezi wa Shawwal kupitia macho ya mwezi.

Nchi kama Saudi Arabia, UAE, Qatar, Kuwait, Uingereza, na Uturuki zilitangaza jana usiku kuwa Ijumaa itakuwa siku ya kwanza ya Shawwal, na kwa hivyo kuanza Idul Fitr.

Kwingine nchi kma Pakistan, Oman, Brunei na Iran zilitangaza Jumamosi kama Eid al-Fitr.

Katika taarifa yake, Ofisi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislam Ayatollah Seyyed Ali Khamenei ilibaini kuwa kama mwezi haukuonekana Alhamisi joini na Ijumaa ni siku ya 30 ya mwezi uliobarikiwa wa Ramadhani.

Ofisi ya marjaa wa Kishia Iraq Ayatullah Ali al-Sistani pia ilitoa taarifa Alhamisi, na kusema kuwa Jumamosi itakuwa siku ya kwanza ya Shawwal.

Katika Siku Kuu ya Idul Fitr kuna Sala ya Jamaa ambayo husaliwa katika uwanja wazi au ukumbi mkubwa.

Waislamu wameamriwa na Mwenyezi Mungu, kama ilivyotajwa katika Qur’ani Tukufu, kutoa sadaqa inayojulikana kama Zakat al-Fitr kabla ya Sala ya Idi.

4135714

Kishikizo: idul fitr ramadhani
captcha