Hafla hiyo ya siku tatu ilivutia wageni 4,750 kutoka nchi 64.
Mikataba kadhaa ya ushirikiano katika nyanja anuwai kama vile kilimo, uundaji wa mashine, vyombo vya habari, na chakula ilifikiwa wakati wa mkutano huo.
Mkutano huo ulifanyika kwa kwa lengo la kuimarisha uhusiano kati ya Russia na Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC). Washiriki katika kikao hicho walijadili masuala ya kifedha, sekta ya ‘Halal’, diplomasia ya vijana, dawa, michezo, tasnia ya ubunifu, uchukuzi na mawasiliano usafirishaji, biashara, na uwekezaji.
Maonyesho ya Halal ya Russia yalifanyika katika hafla hiyo, ambayo kaulimbiu yake kuu lilikuwa "matumizi yenye fahamu".