Kwa mujibu wa Televisheni ya Sky News Arabia, wizara hiyo imesema marufuku ya Umrah iliyotangazwa Machi kutokana na mlipuko wa COVID-10 itaendelea kutekelezwa.
Taarifa hiyo imesema hali ya Ibada ya Umrha itaendelea kutathminiwa kwa mujibu wa taarifa za afya kuhusu janga la COVID-19.
Saudi Arabia bado haijatoa tangazo la mwisho kuhusu kufanyika au kutofanyika Ibada ya Hija mwaka huu ingawa baadhi ya nchi kama vile Indonesia, India na Afrika Kusini zimetangaza kuwa raia wan chi hizo hawatashiriki katika Ibada ya Hija kutokana na janga la COVID-19.