IQNA

Wafanyakazi wa kituo cha kuchapisha Qur'ani Saudia wafutwa kazi

12:37 - September 29, 2016
Habari ID: 3470586
Wafanyakazi wa moja ya mashirika makubwa ya eneo la mashariki mwa Saudia wamefanya maandamano kulalamikia kutolipwa misharahara yao.

Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, wafanyakazi hao wamefanya maandamano hayo kulalamikia kitendo cha kutolipwa mishahara yao kwa miezi sita sasa. Wakati huo huo, Shirika la Kuchapisha Qur'ani nchini Saudia nalo limewafuta kazi wafanyakazi wake 1300 kwa kufilisika.

Wafanyakazi hao waliokuwa wakijishughulisha katika kituo kikubwa cha uchapishaji wa Qur'ani Tukufu cha Mfalme Fahd huko mjini Madina, walikuwa hawajalipwa mishahara yao kwa kipindi cha miezi tisa kabla ya kufutwa kazini. Awali watu hao sanjari na kutakiwa kuwasiliana na idara ya uajiri ya Shirika laOger la nchi hiyo, walitakiwa pia kusaini mkataba wa kuacha kazi.

Kushuka kwa bei ya mafuta, uungaji mkono kifedha kwa makundi ya kigaidi na kitakfiri huko Saudia na Iraq na kadhalika vita vya muda mrefu nchini Yemen ambavyo hadi sasa vimeigharimu Saudia kiasi kikubwa cha fedha, ni mambo ambayo yameufanya utawala wa Aal-Saud, kukabiliwa na matatizo makubwa ya kifedha. Hii ni katika hali ambayo, Mfalme Salman bin Abdulaziz Al Saud ametoa amri ya kukatwa mishahara ya wafanyakazi wote wa serikali kwa ajili ya kuokoa bajeti ya serikali.

Itafahamika kuwa, Saudia ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa ukandamizaji wa wafanyakazi, na kwa mara kadhaa mashirika ya kutetea haki za binaadamu yamekuwa yakiilalamikia serikali ya kifalme ya nchi hiyo na kuitaka iheshimu haki za binaadamu.

Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, wafanyakazi hao wamefanya maandamano hayo kulalamikia kitendo cha kutolipwa mishahara yao kwa miezi sita sasa. Wakati huo huo, Shirika la Kuchapisha Qur'ani nchini Saudia nalo limewafuta kazi wafanyakazi wake 1300 kwa kufilisika.

Wafanyakazi hao waliokuwa wakijishughulisha katika kituo kikubwa cha uchapishaji wa Qur'ani Tukufu cha Mfalme Fahd huko mjini Madina, walikuwa hawajalipwa mishahara yao kwa kipindi cha miezi tisa kabla ya kufutwa kazini. Awali watu hao sanjari na kutakiwa kuwasiliana na idara ya uajiri ya Shirika laOger la nchi hiyo, walitakiwa pia kusaini mkataba wa kuacha kazi.

Kushuka kwa bei ya mafuta, uungaji mkono kifedha kwa makundi ya kigaidi na kitakfiri huko Saudia na Iraq na kadhalika vita vya muda mrefu nchini Yemen ambavyo hadi sasa vimeigharimu Saudia kiasi kikubwa cha fedha, ni mambo ambayo yameufanya utawala wa Aal-Saud, kukabiliwa na matatizo makubwa ya kifedha. Hii ni katika hali ambayo, Mfalme Salman bin Abdulaziz Al Saud ametoa amri ya kukatwa mishahara ya wafanyakazi wote wa serikali kwa ajili ya kuokoa bajeti ya serikali.

Itafahamika kuwa, Saudia ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa ukandamizaji wa wafanyakazi, na kwa mara kadhaa mashirika ya kutetea haki za binaadamu yamekuwa yakiilalamikia serikali ya kifalme ya nchi hiyo na kuitaka iheshimu haki za binaadamu.

Suala linalozidisha matatizo ya kiuchumi ya Saudia mbali na matumizi ya ndani zaidi linahusiana na gharama kubwa za masuala ya kijeshi na sera za vita za watawala wa Riyadh. Kwa sasa Saudi Arabia inashika nafasi ya tatu baada ya Marekani na China katika orodha ya nchi zenye bajeti kubwa zaidi ya masuala ya kijeshi duniani. Mwaka 2014 Saudia ilishika nafasi ya kwanza kati ya nchi zinazonunuasilaha kwa wingi kutoka nje ya nchi. Mwaka huo Watawala wa kifalme wa Saudia walinunua silaha zenye thamani ya dola bilioni 604 kiwango ambacho kiliongezeka kwa asilimia 54 ukilinganisha na mwaka wa kabla yake. Wakati huo huo India ambayo ni miongoni mwa nchi kubwa muhimu duniani iliagiza silaha zenye thamani ya dola bilioni 57.5. 

3461043

Kishikizo: saudia qurani iqna
captcha