Walowezi hao waliingia msikitini chini ya ulinzi mkali wa polisi wa utawala vamizi na wa kikoloni wa Israel.
Polisi wa utawala ghasibu wa Israel waliendelea kuweka vikwazo vya kuwazuia Waislamu Wapalestina kuingia ndani ya msikiti huo.
Wakati huo huo, wito umetolewa kwa Wapalestina wenyeji wa mji Al Quds kujitokeza kwa wingi katika Msikiti wa Al-Aqsa ili kukabiliana na uvamizi wa walowezi wa Kizayuni ambaoo wanatekeleza mpango wa Israel wa Kuyahudisha mji wa Al Quds na Msikiti wa Al Aqsa mjini humo.
Kila siku, isipokuwa siku ya Ijumaa na Jumamosi, Al-Aqsa inakumbwa na mfululizo wa uvamizi wa walowezi, nyakati za asubuhi na jioni. Uvamizi huo ni sehemu ya majaribio ya utawala wa Kizayuni wa Israel kutekeleza njama mpya katika Msikiti wa Al Aqsa kwa kuongeza masaa ambayo Wazayuni wanaruhusiwa kuwa ndani ya msikiti huo yaani kuuhujumu.
Mpango huu ni katika fremu ya utawala wa Kizayuni kuugawa Msikiti wa Al Aqsa kwa mujibu wa kile kinachotajwa kuwa ‘mahala na wakati’
3481420